عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

Those who set the ranks [As-Saaffat] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah Those who set the ranks [As-Saaffat] Ayah 182 Location Maccah Number 37

Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.

Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.

Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.

Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.

Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.

Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki.

Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki.

Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.

Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.

Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.

Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?

Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe

Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!

Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.

Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.

Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.

Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.

Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.

Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.

Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.

Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?.

Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!.

Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.

Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.

Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.

Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.

Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.

Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.