عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

The Pen [Al-Qalam] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah The Pen [Al-Qalam] Ayah 52 Location Maccah Number 68

Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.

Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.

Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.

Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,

Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.

Wala hawakusema: Mungu akipenda!

Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.

Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.